• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI WILAYANI SIKONGE

Imewekwa: March 8th, 2021



MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI WILAYANI SIKONGE

Na.Anna Kapama,

Wilayani Sikonge maadhimisho ya siku ya wanawake ambayo hufanyika kila mwaka ifikapo tarehe 8 mwezi Machi,yamefanyika  katika viwanja vya TASAF kata ya Tutuo, huku Mgeni rasmi akiwa Katibu Tawala wa Wilaya, Renatus Mahimbali ambaye amemuwakilisha Mkuu wa Wilaya. Katibu Tawala amewasisitiza wanawake kugombea nafasi mbalimbali za uongozi huku akiongeza kuwa ufaulu wa wanafunzi wa kike umeongezeka kuonesha kwamba wanawake wanaweza.

Maadhimisho hayo yenye kauli mbiu WANAWAKE KATIKA UONGOZI;CHACHU KUFIKIA  DUNIA YENYE USAWA yalianza kwa maandamano katika Shule ya Msingi Muungano hadi viwanja vya TASAF.

Akizungumza na wananchi waliohudhuria sherehe hizo, Susana Makoye aliyemuwakilisha Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Wilaya, amewaomba wanawake kudumisha upendo katika familia hasa kuheshimu na kuwajibika katika majukumu yao,huku akisisitiza kusameheana ili umoja na mshikamano uweze kudumu katika familia.

Kwa upande wake Mhe.Juma Ikombola, Diwani Kata ya Misheni aliyemuwakilisha Mwenyekiti wa Halmashauri  ya Wilaya amewapongeza wanawake kwa kuwa wameonesha mchango mkubwa katika jamii na katika ngazi za uongozi, na kuongeza kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge haiko nyuma katika kuwawezesha wanawake kwani  imetenga fedha kwa vikundi vya wanawake  wajasiriamali kiasi cha Shilingi Milioni 120.

Nae Mwenyekiti wa CCM Wilaya, Anna Chambala  amewapongeza wanawake kwa kusema mwanamke ni mlezi wa familia, huku akiipongeza Serikali kwa kuwapa nafasi katika uongozi na kuwataka wanawake kushikamana ili kuleta maendeleo endelevu.

Maadhimisho hayo yameambatana na huduma mbalimbali ikiwemo uchangiaji damu pamoja na Elimu ya afya ya Uzazi ambapo wananchi wamejitokeza kuchangia damu na kupata Elimu hiyo ya Afya ya Uzazi.

Historia fupi ya siku ya wanawake duniani ;Waanzilishi wakuu wa siku hii kilikuwa ni chama cha kijamaa kutoka nchini Marekani  kikiongozwa na mwanamke Clara Zetkin ambae alipendekeza wazo hilo katika mkutano wa wanawake uliofanyika mnamo  Februari mwaka 1908 huko COPENHAGEN Nchini Denmark na kuhudhuriwa na wanawake kutoka mataifa mbalimbali Duniani.

 Kwa mara ya kwanza siku ya wanawake Duniani ilisherehekewa  mnamo mwaka 1911 katika mataifa ya Denmark,Australia,Switzerland na Ujerumani ikiwa haijapitishwa rasmi na umoja wa mataifa, na baadae mnamo mwaka 1975 ikapitishwa rasmi na Umoja wa Mataifa kuwa siku ya wanawake Duniani kila ifikapo tarehe 8 mwezi Machi.(source,bbc)

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE YAADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO KWA KUFANYA USAFI

    April 26, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa