• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

MAADHIMISHO YA SERIKALI ZA MITAA SIKONGE

Imewekwa: July 2nd, 2018

MAADHIMISHO YA SERIKALI ZA MITAA SIKONGE

Sherehe za maadhimisho ya Serikali za mitaa hufanyika Julai Mosi ya kila Mwaka. Serikali za mitaa inajumuisha uongozi kuanzia ngazi ya Kitongoji, Kijiji, Kata hadi Wilaya.

Maadhimisho hayo kwa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge yamefanyika katika Kata ya Nyahua kijiji cha Makibo jana. Katika maadhimisho hayo mgeni rasmi alikuwa ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge Mhe. Peter Mihayo Nzalalila.

Aidha, mgeni rasmi aliambatana na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Paschal Ngunda ambaye pia aliambatana na Wakuu wa Idara.

Akimkaribisha mgeni rasmi Mwenyekiti wa Kijiji cha Makibo, Ndogosa lubinza alifurahi sana kwa ujio wa ugeni huu kwa ajili ya maadhimisho hayo na aliwakaribisha sana katika kijiji cha Makibo.

Mheshimiwa diwani wa kata ya Nyahua, Andrea Masanja nae aliwakaribisha Wageni na kutoa changamoto zinazoikabili kata yake ambazo ni kikwazo kikubwa cha maendeleo. " Kata yangu inachangamoto kubwa mbili, kwanza miundombinu ya barabara ni mibovu inakwamisha huduma za kijamii kama afya na shule lakini pia mawasiliano ya mitandao ambayo inatuwezesha kuwasiliana na kutoa taarifa hasa za matukio ya dharua ni shida sana" alizungumza kwa uchungu sana diwani huyo.

Aidha, Mkuu wa Idara ya Utawala na Utumishi, Mrishi ambae pia ni mlezi wa kata hiyo aliwaasa wananchi na kuwataka kushiriki katika shughuli za kimaendeleo ili kuijenga Kata yao kwa manufaa ya jamii na taifa kwa ujumla.

Mgeni rasmi alizungumzia na kusisitiza juu ya majukumu ya viongozi kuanzia ngazi ya kitongoji na kuanza kuwauliza baadhi ya viongozi kama wanayafahamu majukumu yao. Viongozi wengi waliosimamishwa na mgeni rasmi kutaja majukumu yao walifanya vizuri na aliwasifu sana kwa kutambua majukumu yao.

Aidha, mgeni rasmi aliwaasa wafugaji kutoshawishika kutoa rushwa kwa hali yoyote ile na pia viongozi wajiepushe na suala la rushwa na wajikite katika kutoa huduma kwa jamii kwa kufuata taratibu na kanuni. “ Wananchi huduma zote ngazi ya kitongoji hadi kata ni bure, msitowe hela yoyote…” alisema mgeni rasmi.

Pia mgeni rasmi alisisitiza suala la kuwapeleka shule watoto wote wenye umri wa kwenda shule na alisisitiza kuwalinda, kuwajali watoto hasa wa kike. Aliwataka viongozi na walimu kukomesha utoro wa wanafunzi na mimba za utotoni na kukumbushia agizo la Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Agrey Mwanri ambae aliagiza kuwepo kwa maandamano siku ya Julai 2 katika kila kata yenye kauli mbiu ya “Oparesheni Kamata Weka Ndani kwa Kutotii Amri Halali”.

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • UZINDUZI WA SHULE YA MSINGI KININGA - KATA YA IPOLE

    May 09, 2025
  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa