• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YAKAGUA MIRADI MITATU YA UJENZI INAYOTEKELEZWA KATIKA KIPINDI CHA ROBO YA TATU 2023/2024 YENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI 287.9.

Imewekwa: May 14th, 2024

Mhe. Rashid Magope ameongoza wajumbe wa kamati ya fedha,uongozi na mipango kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa  katika kipindi cha robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2023/2024.

Kamati  hiyo imefanya ukaguzi katika mradi wa  ukarabati wa jengo la maenesho ya nanenane lililopo kata ya Ipuli katika manispaa ya Tabora linalogharimu kiasi cha shilingi milioni 18,likihusisha kuziba nyufa,kuweka dari,kupaka rangi ,kusuka nyaya za umeme,kukarabati wa milango,kukarabati mfumo wa maji taka pamoja na kuweka wavu kwenye madirisha,hatua ya mradi imefikia asilimia 40% ya utekelezaji wake.

Vilevile kamati hii imezuru mradi wa ujenzi wa jengo la kufulia katika kituo cha afya Kiyombo kilichopo kata ya Kipili unaogharimu shilingi milioni 35.9.Mradi umefikia asilimia 80%  na upo hatua za mwisho za ukamilishaji.

Mradi mwingine uliokaguliwa ni ujenzi wa vyumba nane vya madarasa na matundu 12 ya vyoo katika shule ya sekondari Kiwere iliyopo kata ya Kitunda wenye gharama ya shilingi milioni 234, ujenzi umefikia asilimia 60% ya utekelezaji na mpaka kufikia  mwishoni mwa mwezi Juni  mwaka 2024 mradi huu utakuwa umekamilika.

Wakiwasilisha ushauri na maoni wajumbe wa kamati hii wamesema dosari zote zilizobainika katika hatua mbalimbali za utekelezaji zirekebishwe na wamemwagiza mhandisi wa ujenzi wilaya ya Sikonge kuhakikisha mapendekezo yote yaliyotolewa yafanyiwe kazi ipasavyo.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge Ndg. Seleman Pandawe amewasihi wote waliokasimishwa madaraka kwa niaba ya mkurugenzi wahakikishe wanatimiza wajibu wao ikiwa ni pamoja na kufuata maagizo yote yanayotolewa na Serikali hususani suala nzima la kuzingatia ununuzi wa umma ufanyike kwa njia ya mfumo wa NeST na wala si vinginevyo.

Akihitimisha ziara hiyo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge Mhe. Rashid Magope amesisitiza kuongeza jitihada na kasi ya ujenzi kwa kuzingatia ubora na umaridadi wa kazi, kwani miradi hiyo inatarajiwa kuja kuzinduliwa na mbio za Mwenge wa Uhuru 2024.

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • UZINDUZI WA SHULE YA MSINGI KININGA - KATA YA IPOLE

    May 09, 2025
  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa