• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE YAPATA HATI INAYORIDHISHA TAARIFA YA UKAGUZI YA MWAKA 2023/2024

Imewekwa: June 14th, 2025

Na Edigar Nkilabo,  Sikonge

Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge imepata Hati inayoridhisha baada ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za serikali CAG kukagua na kuridhishwa na taarifa za fedha ambazo zimeandaliwa kwa usahihi na kwa kuzingatia viwango vya uhasibu vya kimataifa vya uandaaji wa taarifa za fedha (IPSAS)

Akizungumza Wilayani Sikonge katika kikao maalum cha Kamati ya fedha,uongozi na mipango kupitia utekelezaji wa hoja za ukaguzi wa hesabu za mwaka 2023/2024  Mkaguzi Mkuu wa Nje mkoa wa Tabora Hamza Zonga amesema hati hiyo imetolewa na CAG kwa kuwa hakuna jambo lolote kubwa lililobainika na mkaguzi kumfanya atoe hati yenye shaka.

“Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge ilifanyiwa ukaguzi wa Hesabu na CAG kwa mwaka ulioishia tarehe 30Juni, 2024 na kupata hati inayoridhisha hata hivyo haimaanishi kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge ina mfumo wa udhibiti wa ndani wenye ufanisi wa asilimia mia moja”amesema.

Kwa upande wake katibu tawala wa mkoa wa Tabora Dkt.John Mboya amewataka wakuu wa Idara na vitengo kutoa ushirikiano kwa mtunza hazina DT na mkaguzi wa ndani DIA

 “Nimeona taarifa ya ukaguzi wa mwaka 2023/2024 ilikuwa na jumla ya mapendekezo 46 yaliyokuwa yakihitaji ufuatiliaji.Mapendekezo haya yanajumuisha mapendekezo ya hoja 29 zilizoibuliwa katika ukaguzi  wa hesabu wa mwaka 2023/2024 na hoja 17 za mwaka  wa nyuma katika utekelezaji naona mapendekezo 11 sawa na asilimia 24 yametekelezwa, mapendekezo 35 sawa na asilimia 76 yapo katika utekelezaji hivyo niaagize wataalamu kushirikiana na DT kikamilifu kujibu hoja sio mnaachia wasaidizi wenu”alisema.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge Mhe.Rashid Magope amesema hati inayoridhisha imetokana na utendaji mzuri wa wataalamu katika kusimamia matumizi sahihi ya fedha..

“Nawapongeza wataalamu wetu wamekusanya mapato kwa asilimia 98 hadi mwezi Mei, vivyo hivyo kwenye matumizi wamekuwa wakisimamia matumizi sahihi na kuwezesha hati inayoridhisha licha wa uwepo wa changamoto ndogo ndogo”alisema.

Naye mkuu wa mkoa wa Tabora Mhe.Paul Chacha amesema watumishi wanapaswa kufanya kazi kwa nidhamu na ushirikiano ili kumaliza hoja zilizosalia, si jambo jema kubaki na hoja ambazo zinaweza kufungwa kama zitajibiwa kwa usahihi.

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA UMMA WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE WAPIGWA MSASA JUU YA MATUMIZI YA MFUMO WA E-UTENDAJI (PEPMIS)

    June 25, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE YAPATA HATI INAYORIDHISHA TAARIFA YA UKAGUZI YA MWAKA 2023/2024

    June 14, 2025
  • UBORESHAJI WA HUDUMA ZA AFYA WAPUNGUZA VIFO VYA MAMA NA MTOTO KUTOKA 74% HADI 43% WILAYANI SIKONGE

    June 13, 2025
  • VIJIJI 16 KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE KUNUFAIKA NA PROGRAMU YA UANDAAJI WA MIPANGO YA MATUMIZI YA ARDHI

    June 06, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Matangazo
  • Zabuni
  • Matukio
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa