• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE IMETOA MIKOPO ISIYO NA RIBA KWA VIKUNDI 55 VYA WANAWAKE,VIJANA NA WENYE ULEMAVU.

Imewekwa: January 17th, 2025

Na, Edigar Nkilabo


Halmashauri ya wilaya ya Sikonge imetoa mikopo isiyo na riba ya shilingi 460,499,999 kwa vikundi 55 vya vijana, wanawake na wenye ulemavu ikiwa ni mwendelezo wa juhudi za serikali ya awamu ya sita ya kuwakwamua wananchi kiuchumi kupitia 10 % ya mapato ya ndani yanayotengwa kwa ajili ya kuinua kipato cha makundi hayo.

Mgeni rasmi katika hafla ya uzinduzi wa utoaji mikopo isiyo na rib ani Mkuu wa wilaya ya Sikonge Mhe.Cornel Lucas Magembe ambaye anaipongeza halmashauri ya wilaya ya Sikonge kwa kuendelea kutekeleza ilani ya chama na takwa la kisheria la kutenga 10% ya mapato yake ya ndani kwa ajili ya vikundi vya vijana ,wanawake na wenye ulemavu.

“Fedha hizi ni nyingi halmashauri mmetimiza wajibu wenu nitoe rai kwa vikundi vyote 55 ambavyo vimebahatika kupata mikopo hii isiyo na riba viende vikaanzishe biashara na kuendeleza miradi kama walivyoeleza katika maandiko waliyowasilisha wakati wa maombi ya mkopo ili waweze kujikwamua kiuchumi,kuongeza pato la taifa bila kupata tabu ya mikopo ya kausha damu ambayo imekuwa ikiwaumiza wananchi wengi” Mhe.Magembe.

Aidha mkuu wa wilaya Mhe.Magembe amevitaka vikundi vyote vilivyokopa kurejesha fedha za mikopo hiyo kwa wakati kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa kuweza kutoa fursa kwa vikundi vingine kuomba na kupata fedha hizo ili kutimiza lengo la serikali la kuwawezesha wananchi wote wenye uhitaji kujiendeleza kiuchumi.

Kwa upande wao Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Tito  Ruchagula  na Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Sikonge Mhe.Rashid Magope wamesema serikali imeandaa utaratibu mzuri ambao utasaidia mikopo kurejeshwa kikamilifu huku Katibu wa CCM Wilaya ya Sikonge Ndg.Salum Mgaya akieleza kukoshwa na  utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi CCM ambayo inaelekeza serikali kutenga fedha na kuwawezesha wananchi mitaji ya kuanzisha na kuendeleza biashara kwa manufaa yao na jamii kwa ujumla.

Nao baadhi ya wanufaika wa mikopo hii wanasema fedha hizo zitatumika kubadilisha hali zao za kiuchumi.“Fedha hizi zitanisaidia kuendeleza biashara zetu ambazo zinatupatia fedha ya kujikimu, ninasomesha watoto na kuwapatia mahitaji ya muhimu kwakweli ninaishukuru serikali ya awamu ya sita” Amina Ntalamba.

Jumla ya vikundi 107 viliomba mkopo wa asilimia 10 %  usio na riba huku vikundi 55 pekee vikikidhi vigezo vya kupatiwa mikopo hiyo ambayo itaendelea kutolewa katika dirisha la pili.

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE YAADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO KWA KUFANYA USAFI

    April 26, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa