• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

“CHANJO HII NI SALAMA, CHANJO HII HAIKUZUII KUZAA BALI INAKUSAIDIA KUWA NA UZAZI SALAMA” DC.CORNEL MAGEMBE.

Imewekwa: April 22nd, 2024

Mkuu wa wilaya ya Sikonge Mhe. Cornel Magembe ameongoza zoezi la uzinduzi wa chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi lililofanyika katika uwanja wa shule ya msingi Mbirani.

Mhe. Magembe ametoa wito kwa wananchi kuitikia chanjo hii hususani kwa walengwa ambao ni  wasichana wenye umri kuanzia miaka 9 hadi 14 ili kuiepusha jamii na ugonjwa hatari wa saratani ya mlango wa kizazi ambao huwapata akinamama wengi nchini.“Ninawaomba sana muipokee chanjo hii,unapopata chanjo hii unakuwa na uhakika wa kutopata saratani ya mlango wa kizazi,lakini pia tunaliepusha taifa kuwa na wagonjwa wengi wa kansa hivyo kuiepusha serikali kughalamika kununua dawa za kutibu kansa.”amesema Mhe. Magembe.

Kwa upande wake mkuu wa divisheni ya afya,ustawi wa jamii na lishe Dkt. Christopher Nyalu amesema zoezi hili linalenga wasichana wenye umri wa miaka 9 hadi 14 ili kuwakinga na ugonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi,Dkt.Nyalu ametoa wito kwa jamii kuitikia zoezi hili kwa usalama wa kizazi cha taifa,ameongeza kuwa wilaya ya Sikonge inatarajia kuwapatia chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi wasichana 30,307 na kwa kituo cha shule ya msingi Mbirani wanatarajia kuchanja wasichana 396 kufikia Aprili 24,2024, na zoezi hili linaloongozwa na kauli mbiu isemayo “Jamiii liyopata chanjo,Jamii yenye Afya” litaendelea kutolewa katika vituo vyote vya  afya na zahanati.

Akitoa salamu na kufunga uzinduzi huo, diwani wa kata ya Sikonge Mhe. Peter Nzalalila amemshukuru Mkuu wa Wilaya ya Sikonge kwa kuchagua kata ya Sikonge kufanyia zoezi hili la uzinduzi wa chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi na kuishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa juhudi hizi kubwa za kughalamia chanjo hii ambayo ni ghali na kuileta kwa wananchi bila ghalama yoyote.

Saratani ya mlango wa kizazi inasababishwa na virusi vya HPV (Human papilloma virus),mpaka sasa zimekwisha ripotiwa kesi  660000 za wagonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi duniani kote na saratani hii imekwisha sababisha vifo 350000 duniani kote kufikia mwaka 2022,ugonjwa huu huwaathiri wanawake pekee na wala hauna tiba mahususi  isipokuwa unayokinga mahususi inayotolewa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzani bure.


Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • UZINDUZI WA SHULE YA MSINGI KININGA - KATA YA IPOLE

    May 09, 2025
  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa