• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

BENKI KUU YA TANZANIA YATOA ELIMU KUHUSU NOTI ZA TANZANIA

Imewekwa: May 12th, 2021

BENKI KUU YA TANZANIA (BOT) WATOA ELIMU WILAYANI SIKONGE KUHUSU NOTI ZA TANZANIA

Tarehe 12.5.2021


 _Na. Anna Kapama_ - Sikonge


Wakizungumza na wananchi katika kitongoji cha madukani maafisa hao wa BOT wametoa elimu hiyo ikiwa ni pamoja na alama zinazopatikana katika noti za Tanzania kutokana na uwepo wa watu wanaotengeneza noti bandia.


Meneja msaidizi Idara ya Uhusiano Vicky Msina amesema ni muhimu kwa wananchi kutambua alama muhimu zinazopatikana katika noti halali za Tanzania ili kuepuka utapeli wa kupewa noti za bandia hasa katika kipindi hiki cha ununuaji na uuzaji wa mazao na mifugo kutoka kwa wakulima na wafugaji.


Msina ameongeza kuwa ni vema kwa wafanya biashara kuwa na vifaa vinavyoweza kutambua noti halali  na bandia ambavyo ni pamoja na taa maalumu zenye mwanga wa zambarau (ultraviolet light bulb) kwa kuwa taa hizo zina uwezo wa kutambua alama muhimu zilizo katika noti halali ambazo si rahisi kuzibaini kwa macho ya binadamu pasipo vifaa hivyo.


Kwa upande wake Lilian Silaa ambae ni mmoja wa waliotoa Elimu hiyo amewataka wananchi wa Sikonge kutoa taarifa katika vyombo vya usalama au kwa viongozi walio katika Serikali za mitaa mara wanapobaini kuwa wana  noti hizo ili kuepuka mkono wa sheria wanapobainika. Lakini pia amewaasa wananchi wa Sikonge hasa wafanya biashara wakubwa na wauzaji wa mazao  kutopendelea kupokea fedha taslimu mkononi badala yake watumie njia ya benki na huduma zingine za kifedha kama Airtel money,Tigopesa,M-pesa na zingine ili kuepuka kuchomekewa noti za bandia lakini pia kuepuka hatari ya kuporwa fedha zao.


Katika upande wa utunzaji wa noti za Tanzania watumishi hao wamewashauri wananchi kuzingatia utunzaji wa noti hizo kwa kuepuka kuzishika katika hali ya unyevu,kuzikunjakunja  maana kwa kuzitunza zitaweza kudumu kwa muda mrefu zaidi na kuepuka hasara ambazo Tanzania hupata kutokana kuwapo kwa noti nyingi chakavu zisizoweza kutumika tena.


Maafisa hao wa  BOT wameendelea kutoa elimu kwa  maeneo mbalimbali katika mikoa yote ya Tanzania  ikiwa ni miongoni mwa  majukumu yao kwa Umma.

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • UZINDUZI WA SHULE YA MSINGI KININGA - KATA YA IPOLE

    May 09, 2025
  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa