• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

KAMATI YA SIASA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO-SIKONGE

Imewekwa: August 19th, 2021

KAMATI YA SIASA MKOA WA TABORA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO-SIKONGE.

Kamati ya Siasa Mkoa wa Tabora imefanya ziara na kukagua miradi miwili ya maendeleo Wilayani Sikonge ikiwa ni miongoni mwa majukumu ya kutekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi(CCM).

Kamati hiyo ikiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Balozi.Dkt Batilda Buriani imekagua ukarabati na ujenzi wa baadhi ya majengo katika  Chuo cha Maendeleo ya Jamii(FDC) pamoja na Kiwanda cha kati cha kuchakata Mazao ya Nyuki.

Akisoma taarifa ya Ukarabati na Ujenzi wa majengo likiwemo bwalo la chakula,Mkuu wa Chuo hicho amesema mradi huo umegharimu Tsh.milioni 592.4 na kuongeza kuwa baada ya kukamilika kwake umesaidia kuongeza wanafunzi kutoka wanafunzi 92 hadi 217.

Naye Mwenyekiti wa CCM Mkoa Hassan Mwakasubi amewataka wasimamizi wa Miradi hiyo kuwa waaminifu ili kutimiza azma ya kuleta maendeleo kwa wananchi huku akiwashauri kuyatunza mazingira na miundombinu ili iweze kudumu kwa Muda mrefu.

Kwa Upande wake mjumbe wa kamati ya Siasa Maimuna Abasi amewashauri viongozi wa Chuo hicho kutoa elimu kwa wananchi hasa vijijini  ili waweze kuja kupata elimu ya ufundi hatimaye wakajiajiri.

Katika mradi wa ujenzi wa kiwanda cha Kuchakata na kufungasha mazao ya nyuki Mwenyekiti wa CCM Mkoa amewapongeza kwa hatua waliyofikia huku Mwenyekiti wa CCM mkoa amewataka viongozi na wasimamizi wa mradi huo kusimamia vyema vyama vya wafugaji wa nyuki ikiwemo kuwwpatia elimu ya ufugaji bora wa nyuki,kuwakopesha mizinga na kuhakikisha wanapata soko la uhakika katika kiwanda hicho ili waweze kunufaika na mradi huo.

Kiwanda hicho kinatarajia kutoa ajira za kudumu 22 kwa wananchi,na kuongeza kipato  kwa wafugaji wa nyuki ambao watauza mazao ya nyuki katika kiwanda hicho.

Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Sikonge  Anna Chambala ameiomba kamati hiyo kuwasaidia katika kuhakikisha wafugaji nyuki wanapata maeneo ambayo watafuga kutokana na changamoto ya baadhi ya wafugaji kupata vibali katika maeneo ya misitu. 

Katika hatua nyingine Kamati ya siasa mkoa wa Tabora ambayo iliongozana na viongozi mbalimbali  wa wilaya hiyo akiwemo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Sikonge  na wajumbe wengine wa kamati hiyo wameridhishwa na hatua  iliyofikiwa ya ujenzi wa  kiwanda hicho cha kati cha uchakataji na usindikaji wa mazao ya nyuki.

Nae Kaimu Mkurugenzi Yusuph Hamza  ameipongeza Serikali ya awamu ya sita kwa kuwapatia fedha kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda hicho na kuongeza kuwa kitasaidia kuongeza ajira na kuinua uchumi wa wananchi wa Sikonge na maeneo mengine pamoja na kuongeza pato la taifa na kuwa Kiwanda hicho kilicho katika hatua ya kukamilishwa kitakuwa na uwezo wa kuchakata tani nane kwa siku na tani elfu mbili miamoja na nne kwa mwaka.

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • UZINDUZI WA SHULE YA MSINGI KININGA - KATA YA IPOLE

    May 09, 2025
  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa